Hot story in Town: MAN UNITED YAKWAA KISIKI
#htmlcaption1 Go UP! Pure Javascript. No jQuery. No flash. #htmlcaption2 Stay Connected

Tuesday, October 21, 2014

MAN UNITED YAKWAA KISIKI

Mchezaji wa Manchester United, Marouane Fellaini (kushoto) akijiandaa kufunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza dakika chache baada ya kuingia kutokea benchi akitoka Ander Herrera usiku wa kuamkia leo.
Saido Berahino akifunga bao la pili Westbromwich Albion kwa timu yale dakika ya 66 kipindi cha pili.
Blind's (katikati) akishangilia bao lake baada ya kusawazisha dakika tatu kabla ya mchezo kumalizika.
Kocha Mkuu wa Manchester Utd, Louis van Gaal.

Ligi kuu ya England imeendelea jana usiku ambapo Manchester United ilijikuta ikibanwa mbavu na kushindwa kufurukuta ugenini kwa Westbromwich Albion na kutoka sare ya mabao 2-2 licha kwamba ilitawala mchezo huo.

Mchezo huo wa pekee kwa ratiba ya ligi hiyo ulishuhudiwa Man United ikishindwa kupata walau ushindi wake wa kwanza nje ya uwanja wake wa nyumbani tangu timu hiyo iwe chini ya kocha Louis Van Gaal.

Ni bao la Daley Blind katika dakika za mwisho za mchezo ambalo limeiokoa Manchester United kuzama katika mpambano huo. Awali Stephane Sessegnon wa Westbrom aliitungua United kwa bao la mapema kabla ya Marouane Fellaini aliyeingia kipindi cha pili kusawazisha muda mfupi tu baada ya kuingia uwanjani.

Mshambuliaji kijana Saido Berahino aliipatia Westbrom goli la pili ambalo lilidumu hadi pale Blind aliposawazisha na kuinusuru United na kichapo katika mtanange huo uliochezeshwa na mwamuzi Mike Dean.

No comments:

Post a Comment