Hot story in Town: 2014
#htmlcaption1 Go UP! Pure Javascript. No jQuery. No flash. #htmlcaption2 Stay Connected

Thursday, November 13, 2014

BEBI MPYA WA DIAMOND AIKUMBUKA BONGO? AU?


Dakika chache baada ya kuondoka Bongo na kukwaa pipa, bebi mpya wa Diamond, Zari 'The Boss Lady' akiwa ndani ya ndege alionekana mwenye mawazo mazito katika picha alizotupia juzi kwenye fan page yake ya Face Book na Instagram ikisindikizwa na maneno: " miss you already TZ.....deep Mawazu....". Imedaiwa na wadau alikuwa anaamanisha kumkumbuka 'Sukari ya Warembo' zaidi kuliko TZ.....!

PICHA ZA UTUPU ZA KIM KARDASHIAN ZAPAMBA INTANET, JARIDA

Picha ya Kim Kardashian inayomwonyesha nusu mtu na nusu mnyama.
Picha halisi iliyowekwa kwenye Intanet.…

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AIWAKILISHA TANZANIA KWENYE MAZISHI YA RAIS SATA WA ZAMBIA NOV 11, 2014


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Rais wa Zambia Marehemu Michael Chilufya Sata Ikulu mjini Lusaka Zambia Novemba 11,2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal wa kwanza (kushoto) akiwa na Rais Mstaafu wa Zambia Mhe. Rupia Banda, Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta, Rais wa Msumbiji Mhe. Ermando Guebuza na Kaimu Rais wa Zambia Dkt. Guy Scott kwenye Misa Maalum ya kuaga mwili wa Rais Michael Sata iliyofanyika Novemba 11,2014 kwenye Uwanja wa Taifa mjini Lusaka Zambia.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akizungumza na Katibu Mkuu wa Chama Tawala cha PF Mhe. A.B. Chikwanda kwenye Viwanja vya Ubalozini katika Makaburi ya Viongozi wa Kitaifa wakati mazishi ya Rais wa Zambia Marehemu Michael Chilufya Sata yaliyofanyika Novemba 11,2014 kwenye uwanja wa Taifa mjini Lusaka Zambia.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akimfariji Rais mstaafu wa kwanza Zambia Dkt. Keneth Kaunda mara baada ya kumalizika maziko ya Rais wa Zambia Marehemu Michael Chilufya Sata kwenye Viwanja vya Ubalozini katika Makaburi ya Viongozi wa Kitaifa yaliyofanyika Novemba 11,2014 mjini Lusaka Zambia.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akimfariji Rais mstaafu wa Zambia Mhe. Ruphia Banda baada ya kumalizika mazishi ya Rais wa Zambia Marehemu Michael Chilufya Sata kwenye Viwanja vya Ubalozini katika Makaburi ya Viongozi wa Kitaifa yaliyofanyika Novemba 11,2014. katikati Rais mstaafu wa kwanza wa Zambia Dkt. Keneth Kaunda. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisaini kitabu cha maombolezo ya Rais wa Zambia Marehemu Michael Chilufya Sata kwenye Viwanja vya Ubalozini katika Makaburi ya Viongozi wa Kitaifa yaliyofanyika  Novemba 11,2014.
(Picha na OMR)

DAKTARI ALIYESABABISHA VIFO VYA WATU 13 INDIA MBARONI


Dk. RK Gupta aliyetiwa mbaroni.
DAKTARI anayehusishwa na tukio la vifo vya watu 13 katika kituo cha kutoa huduma ya kuzuia uzazi kwa njia ya upasuaji jimboni Chattisgarh nchini India, Dk. RK Gupta ametiwa mbaroni.



Baadhi ya akina mama waliofanyiwa upasuaji wakiwa hospitali.
Dk Gupta na msaidizi wake waliwafanyia upasuaji wananawake 83 katika kijiji cha Pendari ndani ya saa 3 Jumamosi iliyopita na kusababisha vifo 13 huku wengi wakiwa wamelazwa hospitali, 20 kati yao wakiwa katika hali mbaya.

Rais wa India, Ram Avtar aliyempoteza mke wake aitwaye, Nem Bai akiomboleza na wanaye huko Bilaspur, Chattisgarh.


Ndugu na jamaa wakiomboleza kifo cha mama mmoja aliyefariki baada ya upasuaji huo.

Maandamano yamefanyika baada ya tukio hilo la vifo, huku serikali ya Jimbo la Chhattisgarh ikitoa amri ya kufanyika kwa uchunguzi.Serikali nchini humo inamtaka daktari mmoja kutoa huduma ya upasuaji kwa watu 35 tu kwa siku.

WIMBO MPYA WA NAY WA MITEGO 'AKADUMBA'


DIAMOND KUWABURUDISHA WATANZANIA PARTY YA UHURU WASHINGTON DC AKISINDIKIZWA NA 'TANZANIA ALL STARS NUNUA TICKET YAKO MAPEMA ZIKO LIMITED !!!!

TANZANIA ALL STARS -WIMBO MAALUMU WA MIAKA 53 YA UHURU 
$100 (INCLUSIVE)
3 COURSE  DINNER
BOTTLE OF CHAMPAGNE PER TABLE
LIVE ENTERTAINMENT
CELEB AFRICA TV RED CARPET COVERAGE
RE KNOWN PROFESSIONAL PHOTOGRAPHER 
FREE PARKING
CASH BAR
SPONSORSHIP  LEVELS STILL AVAILABLE 
TICKET ZINAPATIKANA
SAFARI RESTAURANT
4306 GEORGIA AVENUE,NW
WASHINGTON,DC,20011
OR
ONLINE
OR
CALL
301-661-6207
240-764-9970
202-830-8970
*************************************
**************************************

NDG. JERRY SILAA AENDELEA NA ZIARA YAKE MKOANI SIMIYU


Mjumbe wa Kamati kuu ya CCM na mlezi wa mkoa wa Simiyu Jerry Silaa akiongea na wananchi wa kijiji cha Mwamhongo wilayani Meatu, mkoa wa Simiyu. Ndg. Jerry Silaa amechangia mabati 50 kusaidia ujenzi wa zahanati katika kijiji cha Mwamhongo kata ya Mwasengela kilometa 94 toka makao makuu ya Wilaya ya Meatu. Ndg.Jerry amekuwa kiongozi wa kwanza wa Chama chochote wa ngazi ya Taifa kukanyaga ardhi ya Kijiji hiki.
Mjumbe wa Kamati kuu ya CCM Jerry Silaa ambaye ni Mlezi wa mkoa wa simiyu leo katika siku ya sita akikagua utekelezaji wa ahadi ya Mhe Rais Dr.Jakaya Kikwete ya ujenzi wa barabara za lami kilometa 3 kwenye mji wa Mwanhuzi makao makuu ya Wilaya ya Meatu. Kazi imefanyika kwa asilimia 40  na itakamilika mwezi wa tatu mwakani.
Ujenzi wa barabara za lami kilometa 3 kwenye mji wa Mwanhuzi makao makuu ya Wilaya ya Meatu. Kazi imefanyika kwa asilimia 40  na itakamilika mwezi wa tatu mwakani.
Kazi za ujenzi wa barabara za lami kilometa 3 kwenye mji wa Mwanhuzi makao makuu ya Wilaya ya Meatu zikiendelea.

THE RICHEST PEOPLE IN AFRICA: MOHAMMED DEWJI NAMED YOUNGEST BILLIONAIRE IN AFRICA


24. Mohammed Dewji
Net Worth: $2 BILLION
Industry: Diversified
Country of Citizenship: Tanzania
Age: 39
Number of Jobs Created: 16,800
Mohammed Dewji has seen his net worth rise considerably over the past year as his MeTL group, a conglomerate in 11 countries with interests in trade, FMCG and manufacturing, undergoes significant expansion.

MWANAMUZIKI GEEZ MABOVU AFARIKI DUNIA

Ahmed Ally Upete 'Geez Mabovu' enzi za uhai wake.

MWANAMUZIKI wa Hip Hop nchini, Ahmed Ally Upete 'Geez Mabovu' amefariki dunia jana usiku akiwa mkoani Iringa alikokwenda wiki mbili zilizopita akitokea jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa bwana Dennis ambaye alikuwa mtu wa karibu wa Geez Mabovu amethibitisha kuhusu kifo hicho na kusema rapa huyo aliondoka Dar kwenda Iringa akiwa kwenye hali ambayo sio nzuri kiafya. Marehemu Geez Mabovu anatarajiwa kuzikwa leo Novemba 13, 2014.

Mwenyezi Mungu ailze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN

Wednesday, October 22, 2014

TANZANIA YAWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUU WA NNE WA MASWALA YA USALAMA MITANDAO

 KATIBU MKUU WIZARA YA SAYANSI MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA (PROF. PATRICK MAKUNGU) AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI JUU YA WARSHA YA USALAMA MITANDAO AMBAPO TANZANIA IMEKUA MWENYEJI WAKE.
 MKURUGENZI MKUU WA COSTECH NCHINI (DR. HASSAN MSHINDA) AKITOA MANENO MACHACHE KATIKA UFUNGUZI WA WARHA HIYO.
 WASHIRIKI  KUTOKA KATIKA MATAIFA MBALI MBALI WAKIENDELEA NA WARSHA.
 WASHIRIKI  KUTOKA KATIKA MATAIFA MBALI MBALI WAKIENDELEA NA WARSHA.
 PICHA YA PAMOJA NJE YA UKUMBI WA MKUTANO

MHARIRI WA WASHINGTON POST AFARIKI

Mhariri wa zamani wa gazeti la Washington Post, Ben Bradlee enzi za uhai wake.

Mhariri wa zamani wa gazeti la Washington Post,  Ben Bradlee aliyeongoza uhariri wa kashfa ya Watergate miaka ya 70 na iliyosababisha Rais Richard Nixon kuachia ngazi amefariki akiwa na miaka 93.
Ben aliwahamasisha waandishi wawili wa habari Bob Woodward na Carl Bernstein kufuatilia kashfa hiyo ambayo Rais pia alijikuta akihusika.
Rais wa Marekani, Barack Obama akimvalisha medali ya Uhuru, Ben Bradlee.

Habari iliyochapishwa na gazeti hilo baadae ilionekana pia katika filamu na hivyo kumpa umaarufu mkubwa sana mwandishi huyu nguli.
Ben Bradlee hadi anakumbwa na mauti amekuwa ni miongoni mwa watu wanaohesabika kufanya kazi zenye tunu na hasa uadilifu aliouonyesha, Bwana alitoa na sasa amtwaa Amen.
Mwaka 1971, Bradlee (kulia), akiwa na Katharine Graham (kushoto).

Tuesday, October 21, 2014

MAN UNITED YAKWAA KISIKI

Mchezaji wa Manchester United, Marouane Fellaini (kushoto) akijiandaa kufunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza dakika chache baada ya kuingia kutokea benchi akitoka Ander Herrera usiku wa kuamkia leo.
Saido Berahino akifunga bao la pili Westbromwich Albion kwa timu yale dakika ya 66 kipindi cha pili.
Blind's (katikati) akishangilia bao lake baada ya kusawazisha dakika tatu kabla ya mchezo kumalizika.
Kocha Mkuu wa Manchester Utd, Louis van Gaal.

Ligi kuu ya England imeendelea jana usiku ambapo Manchester United ilijikuta ikibanwa mbavu na kushindwa kufurukuta ugenini kwa Westbromwich Albion na kutoka sare ya mabao 2-2 licha kwamba ilitawala mchezo huo.

Mchezo huo wa pekee kwa ratiba ya ligi hiyo ulishuhudiwa Man United ikishindwa kupata walau ushindi wake wa kwanza nje ya uwanja wake wa nyumbani tangu timu hiyo iwe chini ya kocha Louis Van Gaal.

Ni bao la Daley Blind katika dakika za mwisho za mchezo ambalo limeiokoa Manchester United kuzama katika mpambano huo. Awali Stephane Sessegnon wa Westbrom aliitungua United kwa bao la mapema kabla ya Marouane Fellaini aliyeingia kipindi cha pili kusawazisha muda mfupi tu baada ya kuingia uwanjani.

Mshambuliaji kijana Saido Berahino aliipatia Westbrom goli la pili ambalo lilidumu hadi pale Blind aliposawazisha na kuinusuru United na kichapo katika mtanange huo uliochezeshwa na mwamuzi Mike Dean.

MIL.25 ZATUMIKA KILA MWAKA KUSAFISHA MAZINGIRA MBUGA YA MIKUMI


Wanachama wa Mtandao wa Habari za Kijamii Tanzania (Mhakita), wakifanya usafi katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya tamasha la Ujirani Mwema, wilayani Kilosa mkoani Morogoro, hivi juzi. Picha na Mpigapicha Wetu.
KIASI cha sh milioni 25 hutumika kila mwaka katika hifadhi ya Taifa ya Mikumi iliyopo wilayani Kilosa mkoani Morogoro kwa ajili ya shughuli za usafi wa mazingira na kuhudumia wanyama wanaogongwa katika barabara kuu iendayo Iringa na Morogoro inayopita katika hifadhi hiyo.

Kaimu mkuu wa hifadhi hiyo Dattomax Selanyika ,alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi habari waliotembelea katika hifadhi hiyo na kupata fulsa ya kufanya usafi wa mazingira kwa lengo la kupinga masuala ya ujangili kupitia mtandao wa habari za kijamii  Tanzania MHAKITA.

Alisema kati ya fedha hizo milioni 12.5 hutumika kwaajili ya uokotaji wa takataka zinazotupwa na wasafiri wanaotumia barabara hiyo.‘’ Usafi huo hufanywa na vibarua kuanzia eneo la Doma hadi Mikumi umbali wa kilomita 50, na shughuli hiyo hufanywa mara tatu kwa wiki’’ alisema Selanyika.
Aidha alisema katika maeneo yaliowekwa matuta ili magari yaweze kupunguza mwendo kutokana na kuwa ni vivuko vya wanyama pamegeuzwa ndio sehemu ya kutupa takataka kwa wasafiri hao.Alisema utupaji wa takataka katika hifadhi hiyo una madhara makubwa kwa wanyama kwani baadhi ya takataka husababisha wanyama kupoteza maisha wakizila.

Hata hivyo alisema kumekuwa na tabia ya baadhi ya madereva kwenda mwenzo kasi katika hifadhi, hiyo kinyume na sheria na kwamba kusababisha kuwagonga wanyama.Kwa upande wake mkuu wa idara ya ikologia wa hifadhi hiyo Crispin mwinuka alisema idadi ya wanyama wanaogongwa katika hifadhi hiyo wamekuwa wakiongezeka mwaka hadi mwaka ambapo katika kipindi cha miaka 2009 hadi 2013 jumla ya wanyama 604 waligongwa katika barabara hiyo na kupoteza maisha.

Alisema mwaka 2012 wanyama waliogongwa walikuwa 111 huku mwaka 2014 walikuwa 132.Pia alisema katika kipindi hicho hicho jumla ya kilogramu 21,907.80 zilitupwa katika hifadhi hiyo na kusababisha hifadhi hiyo kuingia hasara kubwa katika kuokota taka hizo.Aliwataka wasafiri wanaotumia barabara hiyo kujenga tabia ya kuweka vifaa vya kuhifadhia takataka katika vyombo vya usafiri ili kuepusha tatizo hilo.

PISTORIOUS AFUNGWA MIAKA 5

Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius amehukumiwa jela miaka 5 baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp.

Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius amehukumiwa jela miaka 5 baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp.
Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius akiwa na mpenzi wake Reeva Steenkamp enzi za uhai wake.

Hii ni baada ya mwanariadha huyo mlemavu kupatikana na hatia ya kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp mwaka uliopita bila ya kukusudia.
Jaji aliyetoa hukumu hiyo,Thokozile Masipa,alianza kutoa kauli yake ya mwisho kabla ya kutoa hukumu saa mbili na nusu asubuhi na akasema ni changamoto kubwa kwake kupata adhabu ambayo itaridhisha pande zote kwenye kesi hiyo.
Jaji aliyetoa hukumu hiyo,Thokozile Masipa.

Upande wa mashitaka ulitaka mwanariadha huyo kupewa kifungo cha miaka 10 gerezani baada ya kupatikana na makosa ya kuua bila kukusudia.
Pistorius alisema kuwa alifyatua risasi baada ya kudhani kuwa jambazi alikuwa amevamia nyumba yake.
Upande wa mashitaka unasisitiza afungwe jela wakati wakili wa Pistorius wakimtaka jaji ampe kifgungo cha nyumbani cha miaka mitatu na pia apewe usaidizi na ushauri wa kubadili tabia yake

Y-P WA TMK AFARIKI DUNIA


Wasanii wa Wanaume Family, kutoka kushoto, Dogo Aslay, Stiko na Yesaya Ambilikile YP (kulia) wakiwa katika pozi.
 Msanii wa kundi la TMK Wanaume Family,Yesaya Ambilikile ‘ Y- P’ amefariki dunia usiku wa leo katika Hospitali ya Temeke baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kifua.
Akizungumza na mtandao huu Kiongozi wa kundi hilo, Said Fela, amethibitisha msiba huo na kusema ratiba kamili itatoka leo mchana.

“Mpaka sasa hivi bado hatujaandaa ratiba, tunasubirika kaka yake kwa sababu huyo mtu kafariki usiku hospitali. Kwahiyo ndugu zake wakishakuja ndo watasema tunazikaje, kwa sababu alikuwa mkristo. Kwahiyo kwenye saa 7 mchana ratiba itakuwa tayari,” amesema Fela.

“Tatizo alikuwa anaumwa kifua muda tu, lakini alishaanza kunywa dozi lakini majuzi akazidiwa na tukampeleka hospitali. Jana ndo mwenyezi Mungu kampenda zaidi akamchukua. Wazazi wa marehemu wapo Keko pale, lakini wazazi wake baba na mama walifariki ila ndugu zake wapo, na kuna kibanda waliachiwa na wazazi wake, kwahiyo msiba utakuwa Keko.”

Monday, September 29, 2014

WEMA SEPETU ASHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA

Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ akijiandaa kukata keki yake ya siku yake ya kuzaliwa iliyofanyika usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Kijitonyama.
Wema Isaac Sepetu akiongea na wageni wake (hawapo pichani) kabla ya kukata Ndafu.
Martin Kadinda (kushoto) akimuonesha Wema Sepetu kadi ya gari.
Gari aina ya Nissan Murano alilozawadiwa Wema Sepetu na mpenzi wake Diamond Platnumz.Gari aina ya BMW alilozawadiwa Wema Sepetu na meneja wake Martin Kadinda.

RAIS WA ZANZIBAR MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI CHUO CHA UDAKTARI ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman (katkati) wakisimama wakati wimbo wa taifa ukipigwa katika Mahfali ya Kwanza ya Chuo cha Madaktari Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Taaluma za Sayansi za Afya Mbweni nje ya Mji wa Unguja,(kushoto) Mkuu wa Kitivo cha Tiba DEAN Ulpiano Perez na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dk.Mohamed Saleh Jidawi.
Walimu Madaktari Bingwa katika Chuo cha Madaktari Zanzibar kutoka Nchini CUBA wakiwa katika Mahfali ya Kwanza ya Chuo cha Madaktari Zanzibar yaliyofanyika leo katika viwanja vya Chuo cha Taaluma za Sayansi za Afya Mbweni nje ya Mji wa Unguja mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein.
 
Miongoni mwa wahitimu wa Mafunzo ya Udaktari yaliyotolewa na Mataktari Bingwa kutoka Nchini CUba wakila kiapo cha Utii wa kazi zao mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwa mgeni rasmi katika mahfali ya kwanza yaliyofanyika leo katika viwanja vya Chuo Mbweni nje ya Mji wa Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa zawadi kwa Fatma Mrisho Haji akiwa ni miongoni mwa wanafunzi bora waliopata zawadi katika Mahfali ya Kwanza ya Chuo cha Madaktari Zanzibar yaliyofanyika leo katika viwanja vya Chuo cha Taaluma za Sayansi za Afya Mbweni nje ya Mji wa Unguja (katikati) Dk.Salhia Ali Muhsin Mratibu wa Chuo.