Hot story in Town: RAIS WA ZANZIBAR MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI CHUO CHA UDAKTARI ZANZIBAR
#htmlcaption1 Go UP! Pure Javascript. No jQuery. No flash. #htmlcaption2 Stay Connected

Monday, September 29, 2014

RAIS WA ZANZIBAR MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI CHUO CHA UDAKTARI ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman (katkati) wakisimama wakati wimbo wa taifa ukipigwa katika Mahfali ya Kwanza ya Chuo cha Madaktari Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Taaluma za Sayansi za Afya Mbweni nje ya Mji wa Unguja,(kushoto) Mkuu wa Kitivo cha Tiba DEAN Ulpiano Perez na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dk.Mohamed Saleh Jidawi.
Walimu Madaktari Bingwa katika Chuo cha Madaktari Zanzibar kutoka Nchini CUBA wakiwa katika Mahfali ya Kwanza ya Chuo cha Madaktari Zanzibar yaliyofanyika leo katika viwanja vya Chuo cha Taaluma za Sayansi za Afya Mbweni nje ya Mji wa Unguja mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein.
 
Miongoni mwa wahitimu wa Mafunzo ya Udaktari yaliyotolewa na Mataktari Bingwa kutoka Nchini CUba wakila kiapo cha Utii wa kazi zao mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwa mgeni rasmi katika mahfali ya kwanza yaliyofanyika leo katika viwanja vya Chuo Mbweni nje ya Mji wa Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa zawadi kwa Fatma Mrisho Haji akiwa ni miongoni mwa wanafunzi bora waliopata zawadi katika Mahfali ya Kwanza ya Chuo cha Madaktari Zanzibar yaliyofanyika leo katika viwanja vya Chuo cha Taaluma za Sayansi za Afya Mbweni nje ya Mji wa Unguja (katikati) Dk.Salhia Ali Muhsin Mratibu wa Chuo.

No comments:

Post a Comment