Hot story in Town: MWANAMUZIKI RAPPA MAHIRI KUTOKA NCHINI MAREKANI T.I KUSAMBAZA UPENDO NDANI YA TAMASHA LA FIESTA OKTOBA 18,2014 JIJINI DAR
#htmlcaption1 Go UP! Pure Javascript. No jQuery. No flash. #htmlcaption2 Stay Connected

Wednesday, September 24, 2014

MWANAMUZIKI RAPPA MAHIRI KUTOKA NCHINI MAREKANI T.I KUSAMBAZA UPENDO NDANI YA TAMASHA LA FIESTA OKTOBA 18,2014 JIJINI DAR

Mmojawa Marappa mahiri kutoka nchini  Marekani atambulikae kwa jina la Clifford Joseph Harris,'T.I' ni mmoja wa wanamuziki watakaoangusha bonge la shoo la kusambaza upendo kwa wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake,katika onesho la Fiesta 2014 linalotarajiwa kufanyika ndani ya Viwanja vya Leaders Club   jijini Dar es Salaam Oktoba 18.

T.I
atafanya makamuzi pamoja na wasanii wengine mahiri wa hapa
nchini,watakao pangwa kushusha bonge la burudani kwa wale
watakaobahatika kupangwa kwenye orodha ya Oktoba 18, mwaka huu jijini Dar.

Nguli huyo mwenye albamu nane ambazo ni I'm Serious, Trap Muzik, Urban Legend, King, T.I. vs. T.I.P., Paper Trail, No Mercy na Trouble Man: Heavy Is the Head ambapo nyingi kati yake zimefanya vyema katika soko la muziki.

 T.I ameshinda tuzo tatu za Grammy tangu aanze safari yake ya muziki.Baadhi ya singo kali alizoachia mkali huyo na kufanya vyema ni "Bring Em Out", "What You Know", "Big Shit Poppin' (Do It)", "Swagga Like Us" (FT Kanye West, Jay-Z na Lil Wayne), "Dead and Gone" (FT Justin Timberlake), "Ball" (FT Lil Wayne) na "No Mediocre" (FT Iggy Azalea).


No comments:

Post a Comment